Friday, May 3, 2013

TANGAZO, Mtu mwenye watoto 10 atazawadiwa mil 50;

 Jamaa baada ya kusikia tangazo akamwambia mke wake, sisi tuna watoto 9, ila nikwambie mke wangu mimi nina mtoto 1 nje ya ndoa, naomba tumchukue na huyo wawe 10 tupate hizo ml 50. Mkewe akamwambia poa. Jamaa akaenda kumfata huyo mtoto. Aliporudi hakuwaona wale 9. Akamuuliza mkewe, Watoto wako wapi? Mkewe akajibu, baba zao walipoona tangazo nao wamekuja kuchukua watoto wao, Jamaa akazimia.....!!

USINGIZI MTAMUU

Jamaa flani alikuwa amelala na mkewe.Mara akamuona mtu amesimama kitandani.
Jamaa akafoka,"Toka hapa,we ni nani mpaka unakuja kitandani mwangu?                                      " Yule mtu akajibu,"Mi ni malaika;mtakati fu petro,na hapa sio kitandani mwako uko mbinguni!"
Jamaa,"Huh! Inamaana nimekufa,mbona mi bado kijana...naomba nirudishwe!"
Malaika,"Inawez ekana lakini siwezi kukurudisha kama mtu labda urudi kama mbwa ama kuku."
Jamaa akakumbuka mbwa wanavyopata taabu ya kulinda,akaonel ea arudi kama kuku.
Malaika akamgeuza kuku,akamwambia ajifunze kutaga kabla hajapelekwa duniani.
Akachuchumaa na kuanza kujikamua;yai la kwanza likatoka.akajik amua tena,yai la pili likatoka. Akajik amua tena mara ya tatu.
Wakati yai la tatu linatoka...akas htukia amepigwa konde ikifuatwa na sauti ya hasira ya mkewe, "Pumbavu! Balaa gani hii....unakunya kitandani!

HAHAHAHA KAMA NI WEWE UNGEFANYA NINI?

Jamaa mmoja alipata mchumba akaona ni vyema amtambulishe kwa baba yake, mzee alipomuona tu akasema, "oho huyu ni dada yako ni mtoto wangu huyu nilizaa kipindi niko shule", jamaa akatafuta mchumba mwingine akafanya vile vile lakini mzee akasema "oho ulimufahamu vipi huyu ni dada yako pia" jamaa akaona isiwe shida akatafuta kimwana mwingine, digi alipopelekewa na huyo akasema "aha sasa ww mtoto kwanini unakuwa unakutana na dada zako tu, huyu naye ni dada yako tafuta mwingine ila usimwambie mama yako maana hajui kama nina watoto hawa", 
jamaa akawa na hasira sana akaenda kumpatia story yote mama yake, mama akamwambia "aha hata usijali hao sio dada zako hata kwa damu maana hata wewe huyu sio baba yako ila usimwambie maana hajui ni siri yangu ya muda mrefu, wewe fanya kuchangua unayempenda kati ya hao uoe.

UROHO M-BAYA..

Mwizi alibomoa nyumba akaingia kwenye stoo akaona vinyama kwenye kibakuli vilivyokauka,akaonja kimoja akaona ni kitamu kina chumvi chumvi! Akafurahi akakaa chini akala vyote alipomaliza akaangalia juu ya mlango akaona pameandikwa CHUMBA CHA KUTAHIRIA!! eti unahisi alikula nini?

KWA KUPENDA SIFA.

Wahaya kwa kupenda sifa! leo katika matangazo ya vifo , ndugu Deus Rweyemamu wa masaki anasikitika kutangaza kifo cha mwanawe Joseph Rweyemamu wa Oysterbay, kilichotokea jana Australia baada ya kupaliwa na baga akiwa anaendesha hummer yake mpya. Msiba utafanyika kwa anti yake marekani, taarifa zimfikie Ronaldo Rweyemamu wa Portugal, Koku Kardashian Rweyemamu wa U.S.A, Torres Rweyemamu wa Spain, Walcot Rweyemama wa England, na house girl wao alioko Dubay katika shoping ya mwezi, akamalizia tutawasiliana baadayeeee.

ZIMA MZIKI

Jamaa alipanda tax akamwambia dereva, zima mziki dini hairuhusu kuckliza nyimbo za kidunia kwa sababu wakati wa Yesu hapakuwa na redio, dereva akatii akazma halaf akasimamisha gari na kufungua mlango wa abiria. Jamaa akamuuliza Nini tena? Dereva akajbu 'wakati wa Yesu hakukuwa na tax shuka usubiri punda!

MLEVI DUH!

Kuna MLEVI mmoja alikwenda kanisani ili ABATIZWE kwani alidai kuwa sasa pombe kaiacha.

Basi MCHUNGAJI akamzamisha ndani ya maji mengi na alipoibuka Mchungaji akasema,
"Nimekubatiza kwa jina la Baba na la Mwana na Roho mtakatifu,
Ulikuwa unaitwa NGONYANI sasa umekuwa JOSEPH.

MLEVI aliporudi nyumbani akaichukua CHUPA YA BIA na kuizamisha ndani ya MAJI yaliyokuwa yamejaa kwenye Ndoo, na ilipo ibuka akaiambia,

"Wewe CHUPA ulikuwa ukiitwa SAFARI LAGER na sasa Umekuwa FANTA ORANGE

KISHA AKAINYWA NA KUSEMA AMEN.

SOKWE MTU

Iltokea mitaa ya kati,Mwanaume mmoja alienda kuomba kazi kwenye ZOO,akaambiwa nafasiya kazi ipo lakin hakuna sokwe;hivyo utajifanya sokwe na tutakupa ngozi utavaa.Jamaa siku ya kwanza akavaa walipokuja watalii mambo yalienda vizuri.Siku iliyofuata banda lake liliwekwa juu,jamaa katika kuongeza mbwembwe kwenye kazi yake akawa anarukaruka,kwa bahati mbaya si akaanguka ndani ya banda la simba akawa anapiga kelele;mamaa nakufaaaaaa;Mara yule simba akamwambia "Acha kelele mimi mwenyewe kama wewe,rudi kwenye banda lako haraka kabla watalii hawajaja!!!!!!!!

MLEVI NA MKEWE

Mlevi alimuamsha mkewe usiku amsindikize chooni ili akajisaidie,
Mke akakataa akaondoka mwenyewe,
Aliporejea akaanza kumuhadithia mkewe maajabu aliyoyaona chooni, mkewangu choo chetu kinamaajabu siku hizi,
mke akauliza maajabu gani?
akajibu nilipofungua mlango wa chooni taa imewaka yenyewe kisha kakanipuliza kaubaridi nikajisikia rahaaa na nilipoufunga taa ikazima na kaubaridi kakaisha, mke akasema ''nyoooo mshenzi mkubwa wewe, umeshajisaidia ndani ya friji.

YUPI ANAJUA KUUCHUNA KATI YA HAWA?

Juha:Nilimpigia cm mke wangu akapokea hakusema (hallow)nikauchuna sikuongea mpaka pesa zote zikaisha!
Zoba:iligonga mlango mke wangu hakufungua,hakuniambia karibu nikasimama palepale mpaka kesho yake nikageuza nikaondoka.
Zuzu:Tangu nimuoe mke wangu hajaniita mpenz,nimegoma kulala nae hadi leo miaka 6.Wote wakamwambia we muongo,mbona una watoto wawili?Zuzu akajibu:Mpaka leo sijamuuliza watoto ni wa nani?NIMEUCHUNA TU!!!

FAMILA YA KICHAGA

Mtoto alikwenda kwa mama yake kupeleka malalamiko kwa kile alichotendewa na baba yake na mazungumzo yalikuwa hivi;
Mtoto; Jana nilikwenda kumuomba baba hela ya kusuka akaninyoa nywele {kipara},
Mama; Unabahati sana lau kama ungeomba hela ya whitedent angelikung'oa meno. Lau kama mtoto angelimuomba hela ya wembe wa kukatia kucha unadhani ingelitokea nini?

BALAA LA WATOTO WA CHEKECHEA

Hebu niambie ingekua wewe ni mwalimu wa chekechea halafu vitoto viwili vya chekechea, cha kike na cha kiume vikaja kukuuliza, eti mwalimu, watoto kama sisi tunaweza kupata ujauzito? ''Ukajibu haiwezekani''. Kakiume kikamgeukia mwenzake kakamwambia si nilikuambia usiwe na wasiwasi!!!!! Ungefanyaje?

BARUA YA CHIZI

Jamaa kamkuta chizi anaandika barua .........
JAMAAA; Vp unaituma kwa nani hiyo barua?
CHIZI; Najitumia mwenyewe.
JAMAA; Kwahiyo barua inaujumbe gani?
CHIZI; He! we chizi nn, mimi nitajuajee wakati haijanifikia?

MWALIMU ALIKUTANA NA CHANGAMOTO KAMA SIO CHANGA LA MOTO!

MWALIMU; which crops do we export to euro?
MWANAFUNZI; coffee,
MWALIMU; good, how many types of coffee do we have?
MWANAFUNZI; two types,
MWLIMU; excellent boy! and what are they?
MWANAFUNZI; Coffee Anan and Coffee Olomide,
MWALIMU; safi safi sanaaa, nakuacha cha hivyo hivyo mpaka serikali iniongeze mshahara,!!!!!!!

KIFAA CHA KUKAMATA WEZI

Wamarekani walitengeneza matchine maalum kwa ajili ya kukamatia WIZI, kutokana na mafanikio iliyoyapata kule Amerika wakaamua kuipeleka Urusi, Ndani ya siku 1 ikaonesha wizi 120, wakapeleka na Ghana ndani ya masaa 3 ikabaini wizi 1000,, iliopelekwa China kwa masaa 6 ilifanikisha kukamtwa wizi 2500, Sasa kivumbi iliyoletwa Tanzania, ndani ya robo saa tu Matchine ikaibiwa yenyewe.

JAMAA ALIDONDOKA BANK

Jamaa mmoja alidondoka benk, na haikujulikana ni ni kitu gani kilichomsibu. Watu wakaanza kusema , ''mmwagie maji, mpeni maji, mpeni maji mengi''. Jamaa baada ya kuckia hivyo akaamka akasema ''nyie vp, kama ningelilitaka maji si ningelilianguka idara ya maji, kwani cpajui, hapa nipeni hela tu nyingi, ndo mana nimeangukia hapa benki'' watu mbavu hoi.

MWALIMU ALIKUTANA NA CHANGAMOTO KAMA SIO CHANGA LA MOTO!

MWALIMU; which crops do we export to euro?
MWANAFUNZI; coffee,
MWALIMU; good, how many types of coffee do we have?
MWANAFUNZI; two types,
MWLIMU; excellent boy! and what are they?
MWANAFUNZI; Coffee Anan and Coffee Olomide,
MWALIMU; safi safi sanaaa, nakuacha cha hivyo hivyo mpaka serikali iniongeze mshahara,!!!!!!!

NDANI YA DALADALA''

DEMU;samahani kaka naomba unipakate,
JAMAA; usijali njoo tu nikupakate,
DEMU; haya,
JAMAA; wewe unaonekana ni secretary?
DEMU;ndio, kwani vipi?
JAMAA; vidole vyako laini kweli!
DEMU; asante, nawewe ni fundi magari?
JAMAA; ndio, umejuaje?
DEMU; naona hapa nilipo kaa nainuliwa na kitu kama jeki!
JAMAA; hapana nadhani itakuwa mabonde tu.

MTOTO NA PESA

MTOTO ALIMUULIZA BABA YAKE,
ETI BABA UKIKUTA NOTI YA SHILINGI ELFU KUMI{10,000} NA ELFU TANO {5,000} UTAOKOTA IPI?
BABA; WEMJINGA KWELI NITAOKOTA YA ELFU KUMI {10,000}
MTOTO; WEWE NDIO MJINGA BABA MIMI NITAOKOTA ZOTE.

MCHAGA MSAFIRI

Mchaga 1 alikuwa anasafiri kwenda nje ya nchi, akaita tax impeleke airport akauliza: shngapi kwenda airport, dreva: elfu 30 tu, mchaga: jumla na mzigo itakuwa shngap, dreva: mizgo ni bure, mchaga: basi beba mizgo yangu utangulie nayo mi napanda daladala.!

OPERATION YA MACHO

Jamaa mmoja alifanyiwa operation ya macho baada ya cku 3 akawekewa macho ya paka.Doctor;vp unaona vizuri?Jamaa;NAONA PANYA TU!!!

TAFAKARI NDIO WEWE

Jamaa mmoja alikua amekaa bar akaitazama bia yake kwa zaid ya dakika 20. Akatokea jamaa mmoja baunsa mtemi akaichukua akainywa yote ile bia

jamaa akaanza kulia hata hvo baunsa akamwambia

"usilie bana nilikua nakutania tu nitakununulia nyingine"
...
jamaa akajibu

"hilo sio tatizo ila leo ninamikosi tu, asubuhi kazini nimefukuzwa, baada ya kutoka nje nkakuta gari yangu imeibiwa nikaja zangu bar , nimenunua bia yangu na kuiweka sumu ili nijiue wewe tena umeinywa"

Thursday, May 2, 2013

MUME NA MKE

Mume: Hello baby!
Mke: Hello sweety!
Mume: Nitachelewa kurud leo
Mke: Nishajua uko kwa vijanamke
vyako, ww ni malaya sana cjui ilikuaje ukanioa nakuchukia kama nn? ckupend! ckupend!
Mume: Niko BENKI hapa
Mke: Haa! Ulijuaje kama cna hela,
nitolee laki 1 baby, nakupenda sana
kuliko roho yangu, nakutengea maji
yakuoga sweety. Ucsahau hizo pesa ninunulie na chips kuku mmwaaaa!
Mume: Ni BENKI YA KUCHANGIA DAMU
Mke: Nyoooo waambie wakutoe yote.

HIZI NI TABIA ZA MSICHANA AMBAYE AMEANZA KUKUSALITI

1 Amepunguza mawasiliano. Hi ndiyo njia pekee ya kuweka uhusiano wenu karibu kana alivyokuwa akifanya mwanzo wa mapenzi yenu lakini sasa amepunguza na aishi sababu za kuwa yupo BUSY

2 Anakukwepa kila unapotaka kuonana naye. Hawezi kuonana na wewe kwa sababu utu wa ndani humsutu na hana mapenzi na wewe tena. Hivyo atajarinu kila njia za kukukwepa, kama kusingizia ameyumwa au hana muda

3 ubinafsi. Kama mwanzo mlikuwa mkishare mambo yenu ikiwa simu na siri za maisha yeye ataanza kuweka pasword na pasword ya facebook atabadilisha.

4 hawezi kukuambia hakutaki ila atakuwa hajali uwepo wako hata ukiwepo naye.

5 ayes contact hawezi kuwa na ujasiri wa kuangalia machoni tena kwa sababu ameanza kukusaliti

6 ataanza mashindano ya kuacha kufanya vitu ambavyo vilikuwa ni jukumu lake kukufantia ila sasa atakutegea wewe umfanyiue ukimuuliza kwanini amebadilika atakujibu kwa nini wewe hunifanyii haya.

MAMBO YA KUMFANYIA MSICHANA ILI UWEZE KUMTEKA ASIKUACHE HATA KAMA HUJAMTONGOZA

1. KILA siku usisahau kumsifia kwa kumwambia ni kiasi gani alivyo mzuri. Kumbuka kila msichana anapenda kusifiwa hivyo unapomuambia yeye ni mzuri anaona una mthamini kuliko msichana yeyote awaye.

2. Wakati wowote ukipata nafasi muandikie barua au msg kwenye simu mueleze hisia zako kiasi gani unampenda. Kumbuka wasichana hupenda kusikia zaidi kutoka kwa wapenzi wao ni kiasi gani wanapendwa. Haitakiwi iwe tu katika kipindi cha siku ya wapendanao ndio umuoneshe kuwa unampenda. Muoneshe msichana ni kiasi gani yeye ni muhimu sana kwako.

3. Busu la ghafla na kumshika mkono wakati mkitembea pamoja itamfanya yeye kujisikia raha zaidi. Na wakati mwingine msuprise kwa kumtembelea mara kwa mara hi humfanya akuone wewe ni mtu muhimu pale usipokuwa naye karibu na kumfanya kukuhitaji zaidi ukiwa naye mbali

4. Tambua mahitaji yake. Uwe msaada kwake kipindi ambacho mpenzi wako amekasirika kuwa pale kwa ajili yake na ukimpooza kwa sauti ya upole na mahaba. Utashangazwa sana na kiasi gani msaada huo umeleta mabadiliko kwake. Hakikisha unamsaidia katika shida zake hapa ndipo kuna tatizo kwa wavulana wengi. Mapenzi si pesa lakini kuna kipindi ambacho pesa huitajika kulinda penzi lako. Si msichana anapokuomba pesa ina maana ana nia ya kukuchuna au amekupendea pesa kuna shida nyingine inabidi akuombe wewe tena kwa kukupima kama utakuwa tayari kumsaidia.

5. Mchukue mpenzi wako out mara nyingine itamfanya ajisikie furaha sana kwa sababu wasichana hupenda enjoyment na boyfriend zao. Hii haitamfanya mpenzi wako tu kuwa na furaha bali itawafanya nyie kwa pamoja kujuana na kufahamiana zaidi.

6. Kuwa muwazi kwake usimfiche jambo linalokuhusu. Msichana hupenda kutoa ushauri kwa mtu ampendaye hivyo unapokuwa muwazi atajisikia kuthaminiwa nawe na kukuona umemuamini

7. Ukijiona upo busy sana usithubutu kuacha japo kumpigia simu mara mbili kwa siku hata kama ukishindwa kumpigia wakati upo ofisini darasani au kwingineko hakikisha unapopata nafasi japo ujumbe mfupi wa kumwambia unampenda.

8. Mkumbatie mara kwa mara katika tukio la kumbatizi kuna jambo kubwa sana hutokea. Si kwake tu hata kwako mvulana. Hali ya joto lenu huwaweka pamoja kifikra hata pale msipokuwa pamoja.

9. Epuka maugomvi na hasira za mara kwa mara ukiwa nae. Mwanamke hupenda ustaarabu kwa mtu ambaye yupo serious naye hivyo ukionesha hasira kabla hata hujamtongoza unaweza ukamkosa msichana hivihivi wasichana huwaogopa wavulana wenye hasira na wagomvi kwa sababu hupenda kubembelezwa.

10. Mdekeze. Msichana anapenda kudeka anaenda kudeka sana na kubembelezwa sana hivyo mvulana ukidekewa usikasirike eti huyu msichana kazidi wewe ndio wakati wako wa kumuonesha msuchana wako unampenda mdekeze mpaka aone aibu kudeka siku nyingine. Wasichana wameumbwa kwa jili ya wavulana ndio maana hudeka hii ndiyo silaha pekee na ya mwisho kumpata msichana hata kamasi wako ni wa rafiki yako unaweza ukatumia silaha hii kumpora msichana huyo kwa mwenzio usipojua kudekeza utaachwa pia

KITANDA CHA KAMBA

Jamaa mmoja alikuwa anala kitanda cha KAMBA na Mkewe Na watoto wao walikuwa wanalala chini ya hicho kitanda
Siku moja Jamaa akataka mchezo
Mkewe akamwambia Watoto Bado hawajalala
Jamaa Akabisha.
Ikabidi mkewe Akubali
Jamaa alipoingiza Tu BUNDUKI ikapita kwenye Tundu la Kitanda.
Jamaa akamuuza mkewe, Imeingia?
Watoto wakajibu..
"HAIJAINGIA BABA HII HUKU CHINI"!

KITANDA CHA KAMBA

Jamaa mmoja alikuwa anala kitanda cha KAMBA na Mkewe Na watoto wao walikuwa wanalala chini ya hicho kitanda
Siku moja Jamaa akataka mchezo
Mkewe akamwambia Watoto Bado hawajalala
Jamaa Akabisha.
Ikabidi mkewe Akubali
Jamaa alipoingiza Tu BUNDUKI ikapita kwenye Tundu la Kitanda.
Jamaa akamuuza mkewe, Imeingia?
Watoto wakajibu..
"HAIJAINGIA BABA HII HUKU CHINI"!

MTOTO NA BABA

mtoto;baba nitumie hela ya matumizi huku shuleni hali mbaya la sivyo nitajinyonga
baba; huku nyumbani hali mbaya zaidi kama unajinyonga sawa tu kwasababu utapunguza bajeti. kopa kamba nitakuja kulipa nitakapokuja kuchukua mwili wako. Mungu akulaze mahali pema peponi mwanangu.

MWALIMU KASINZIA DARASANI

MWALIMU Kasinzia darasani , DOGO kamfuata na kumwambia Teacher mbona umetupa zoezi tufanye alafu unasinzia ??

[MWALIMU:] ''hapana mimi sijalala !"

[DOGO]: ''kwani hapa ulikuwa unafanya nini mda huu ? mimi nimekuona umelala''

[MWALIMU:] ''nilikuwa naongea na MUNGU!''

KESHO YAKE

DOGO kasinzia Darasana wakati kipindi linaendelea. MWALIMU akamuamsha
"DOGO, Yani unathubutu kusinzia kwenye kipindi changu?"

[DOGO:] "Hapana mwalimu sijasinzia!"

[MWALIMU:] " Enhee Tuambie Basi ulikuwa unafanya nini ? maana darasa zima limekuona"

[DOGO: ] "nilikuwa naongea na MUNGU na mimi Pia "

MWALIMU Kwa Hasira huku akipiga kelele , " Enhe Hebu Tuambie MUNGU wako Amesemaje ???!?!" maana naona watu mnatafuta Viboko Asubuhi Asubuhi.

[DOGO:] "MUNGU Kasema Hakuongea na wewe Hapo Jana !"

UROHO M-BAYA..

Mwizi alibomoa nyumba akaingia kwenye stoo akaona vinyama kwenye kibakuli vilivyokauka,akaonja kimoja akaona ni kitamu kina chumvi chumvi! Akafurahi akakaa chini akala vyote alipomaliza akaangalia juu ya mlango akaona pameandikwa CHUMBA CHA KUTAHIRIA!! eti unahisi alikula nini?

MTALII NDANI YA BONGO

Mtalii ndani ya Bongo kaona nazi, akawa hajui nini. Akawauliza wenyeji, wakamjibu "Hilo yai la tembo!". Akataka kujua linatotoa vipi. Wakamwambia unalikalia halafu unasugua kwa matako mpaka anatoka tembo. Akarudi nchini kwao, akawambia wanae waanze kusugua. Sugua, sugua wapi! Hamna tembo. Akamwabia mkewe, sugua, sugua wapi! Akaona aingia yeye mzee wa kazi! Akawa kwa nguvu nyingi kichizi! SUGUA, SUGUA, SUGUA, mara ghafla watoto wanaanza kushangilia

"Mkonge, mkonge, mkonge..".. Mzee akazidisha nguvu, mara watoto tena

"Mashkio, Maskiooo, Mashkiooo"..
Mzee akaona bora amchungulie huyo tembo, kucheki vizuri kumbe ilikuwa suruali yake imechanika!!

JAMAA KAINGIA BAR KWA FUJO

JAMAA:lete bia hapa,na kila mmoja humu ndani mpe bia yake,maana nikinywa bia nataka kila mtu anywe bia..
WATU:Haaa..wakapewa bia
JAMAA:Lete mchemsho hapa,na kila mmoja mpe mchemsho wake,mana nikila mchemsho na kila mtu ale mchemsho
WATU:eeee..makofi kwa jamaa..muhudumu akawapa
JAMAA:leta bili hapa na kila mtu mpe bili yake mana ninapolipa bili nataka nione kila mtu analipa bili yake..
WATU: Vilio na mayowe!!

MLEVI NOMAA

Mlevi mmoja alikuwa anapita katika Mkutano wa Injili akasikia Mhubiri wa neno akisema "Msitende dhambi msije mkaenda motoni"

Mlevi akajibu "Nanyinyi huko Peponi mkipewa Mahindi Mabichi msije kuomba moto!"

CHEZEA MADENGE WEWE!

MADENGE alimuuliza MWL; Hivi ukichanganya OMO na FOMA zitatoa POVU!? MWL akajibu kwa HASIRA 'swali gani la KIPUUZI hilo, zitatoa ndio kwa SABABU zote ni SABUNI,!? MADENGE akasema: WEWE ndiyo MPUUZI na MAJIBU yako ni ya KIPUUZI!, bwege WEWE Zitatoaje POVU wakati HATUJAWEKA maji.?DAH! Mwalm hoi.!

MAJINA YA VIMADA

JINSI WANAUME WANAVYO SAVE MAJINA YA VIMADA/MPANGO KANDO KWENYE SIMU ZAO ILIKUKWEPA KUGUNDULIKA NA WAPENZI WAO

1. Mwenye Nyumba
2. Fundi wa viatu
3. Battery low
4. customer care
5. Sister
6. Binamu
7. Josef wa maziwa
8. Boss
9. Daktari wa Meno
10. missed call
11. Mama mdogo

MADENGE

Madenge ali2mwa sokoni na mama yake kununua njegere akiwa njiani anarudi na njegere moja ikadondoka ikabimbilika akasema anhaa kumbe mnajua kutembea! Akamwaga zote chini , mtanikuta nyumbani alipofika nyumbani mama yake akamuliza madenge njegere ziko wapi ? Madenge ziko njiani zinakuja !

Wednesday, April 24, 2013

WAWINDAJI WAWILI

Kuna jamaa wawili,walikwen­da kuwinda, mmoja alikuwa mtaalamu wa kulenga mwingine wa kuchuna, mtaalam wa kuchuna alibaki garini na mwenzake akashuka kuwinda.
Ile anakatiza kichakani mara Simbahuyoooo!o Ikabidi jamaa aanze kukimbia vibaya mno huku akipiga kelele fungua fungua......!?
Mwenzake akafungua mlango wa gari, jammer anakaribia mlangoni huku Simba akiwa nyuma, Simba akamrukia, bahati mbaya jamaa akaanguka chini, Simba akajikuta ndani ya gari, jamaa akaamka haraka akafunga mlango na kumwambia mwenzake..''ANZ­A KUMCHUNA NAKWENDA KULETA MWINGINE''...

TAZAMA HILI BALAA:

Mwalimu kaingia class akiwa na daftari la nukuu, akafunua na kuanza kuandka ubaoni:
Mchele 34,000/=
Unga 26,000/=
Maharage 15000/= Pango 150,000/=
Karo 250,000/=
Mafuta 20,000/=
Mangi Dukani 30,000/=
SACCOS 55,000/=
Mshahara 244,000/= Alipokaa tu akashtuka "Ahaa nimeandika
madeni badala ya
zoezi, Mungu wangu!" Akaanza kufuta Watoto wakapiga kelele
"MWALIMU HATUJAMALIZAAA"

VICHAA WAWILI

Kulikuwa na vichaa wawili wakisimuliana jinsi walivyoota ndoto
Kichaa wa 1: NIMEOTA NIMEENDA MAREKANI
kichaa wa 2: Sasa mwenzio nimeota nimefanya sherehe kubwa basi tukala mipilau,mikuku biriani, na
vinywaji kibao
Kichaa wa1: mh! Unatabia mbaya hata kunikaribisha mwenzio
Kichaa wa 2: SASA WE SI ULIKUWA MAREKANI NINGEKUKARIBISHAJE?

MAMA NA MTOTO WAKE

Mama na mtoto wake wapo kwenye taxi.Wakapita mtaa wakaona wanawake telee wamejipanga barabrani. Mtoto akaauliza "hawa nani?" mama akajibu "hao ni wake wanawasubiri waume zao watoke makazini.

 Dereve taxi akarukia "Sii umwambie mtoto ukweli. Hao ni machangudo wanauza miili yao kwa ajili ya
ngono!" Mtoto akastaajabu sana, akauliza "Dah!sasa mama kama hao badae watoto wao wanakuwa wanafannya kazi gani?"

 Mama kwa hasira akajibu "Wanakuwa madereva wa taxi!"

SMOKE CONVERSATION

LADY: Do you smoke?
MAN: Yes
LADY: How many packs a day?
MAN: 3 packs
LADY: How much per pack
MAN: £10.00
LADY: And how long have you been smoking?
MAN: 15 years
LADY: So 1 pack cost £10.00 and you have 3 packs a day which puts your spending each month at £900. In one year, it would be £10,800 correct?
MAN: Correct
LADY: If in 1 year you spend £10,800 not accounting for inflation, the past 15 years puts your spending at £162,000 correct?
MAN: Correct
LADY: Do you know that if you hadn't smoked, that money could have been put in a step-up interest savings account and after accounting for compound interest for the past 15 years, you could have now bought a Ferrari?
MAN: Do you smoke?
LADY: No
MAN: Where's your Ferrari
then?

MWALIMU MKUU NI NOMAA

Mwalimu mkuu wa skuli ya msingi X alipewa barua kutoka wizarani,

"Tunakuamuru ufunge skuli yako kwasababu haina vyoo. Hivyo basi,mpaka utakapo chimba ndio
masomo yaendelee. Kwa ajili yaafya". Mwalimu alipoona barua akatikisa kichwa halafu akawajibu
kwa swali moja tu!: "Kwani hawa wanafunzi wamekuja KUNYA au wamekuja KUSOMA??"

MAPENZI SIJUI YAKOJE?!!!

Wanaume karibia wote ambao ni Good Looking,wasafi nini,profile picture mashallah,ndevu zimepigwa 'O',ni Maplayer na Hawajali mapenzi...Wale wasio na haiba na mvuto kwa nje,ndio wenye mahaba niue,wako Real na upendo wa dhati na wanacare...Sasa chagua moja,ujivishe Ngata ubebe mzigo wa misumari ukubali kutoka na Player kisa ana mvuto,huku ukijipa mahope kwamba eti Utambadilisha na Kumtuliza ambayo ni ndoto kama kukuta changudoa bikra,au uweke Udiva pembeni kujifanya unapenda mahandsome wenye dimples ili uwaringishie mashosti,''This is my Guy'' ujitome mzimamzima kwa jamaa mwenye sura kama yangu hapa,sura kama umepokea taarifa ya msiba lakini mwenye mahaba tele kwako!
Najua madiva hamuwezi,mnapenda sana Show-Off na ndo maana mnalizwa deile,mnakimbilia sura,bajeti zenu za leso kwa mwaka ni kubwa kuliko bajeti ya Baby Powder!

SWALI LA KIZUSHI !!!

Mwanamke m1 alimwomba mpangaji mwenzie wa kiume ndoo ya kuogea baada ya kumaliza kuoga akamrudishia jamaa ndoo yake.

Baada ya muda dada akakumbuka
alisahau chupi yake kwenye ile ndoo akarudi kwa jamaa ili achukue chupi yake.

Jamaa akamwambia aingie ndani
akachukue wakati, anatoka ndani kwa msela na mume wake anatoka job na kumuona mkewe anatoka geto kwa msela huku ameshika chupi mkononi.......

je ingekua ww ungefanyaje?

HEBU VUTA PICHA,

Ni asubuhi unaamka halafu unakuta umevalishwa pete ya dhahabu kidole cha pili kisha kwenye mto ipo karatasi ina ujumbe unaosomeka:-

"NAKUPENDA SANA KWA PENZIi ULILONIPA UCKU WA LEO NA NIKAAMUA BORA NIKUVISHE HIYO PETE , Ni mm nikupendae "POPOBAWA"

Ama kweli UALIMU kazi ya wito

MWANAFUNZI mmoja hajui kujumlisha+ wala kutoa-
Mwalim katumia njia zote
kumuelimisha lakin wapi Ikabidi
ajaribu njia hii
Mwl: Kwenu mnafuga nin
Mwnfz: Kuku na mbuzi.
Mwl: Mbuzi mnao wangapi?
Mwnfz: 25
Mwl: Mbuzi 25 toa mbuz 5 watabaki
wangapi?
Mwnfz: Unawajua mbuz we2, au unawackia?
Ukimtoa mmoja tu wote wanatoka.
Mwl: mmh! naacha kazi

((((((I HURT MY MOM!!)))))) STORY FUPI ZENYE MAFUNZO MAISHANI

Mama yangu alikuwa na jicho moja, nilikuwa namchukia sana, kwa ufupi alikuwa kero sana kwangu. Mama alikuwa mpishi katika shule niliyokuwa nasoma, ilikuwa ni shule iliyojengwa maalumu kwa ajili ya watoto yatima. Pengine waweza kujiuliza kwa nini nilikuwa nasoma pale wakati nilikuwa na wazazi? Ukweli ni kwamba baba yangu alikuwa amefariki miaka mingi wakati mie bado mtoto mchanga. Mama aliomba kazi ya upishi katika shule ile ili apate pesa za kunitunzia mimi wakati huo maana baada ya kufariki baba ndugu walimpora mali zake zote na kumfukuza katika nyumba yake, hivyo ndiyo sababu iliyopelekea mama kuomba kazi ya upishi katika shule ile ili apate kujikimu kimaisha. Kama nilivyokwambia hapo awali kwamba kutokana na jinsi alivyokuwa mama nilikuwa simpendi kabisa. Mama yangu yeye alikuwa ananipenda sana na alijitahidi kunipenda sana lakini sikujali hayo, kwani alikuwa ananikera sana na ile hali ya kuwa na jicho moja.

Mama alikuwa ananitembelea kila mara wakati wa mapumziko alikuwa akijisikia raha sana kuniona mwanae nikiwa ana furaha wakati wote, lakini tofauti na hapo nilikuwa nakosa amani sana kila alipokuwa akitokea tu. Basi mama wakati mwingine ilimbidi asije kunisalimia maana alikuwa hapendi kuniudhi. Siku moja baada ya juma moja kupita mama alikuja kunitembelea na kutaka kunijulia hali, nilipomwaona tu nikakunja sura kuonyesha kukasirishwa na ule ujio wake. Nikawaza moyoni mwangu na kusema “Hivi huyu mwanamke kwa nini ananifanyia hivi?” ina maana yeye anajisikia raha kunikosesha amani. Mama aliponiona tu alitabasamu na kunifuata ….. mmoja kati ya wanafunzi wangu alicheka na kusema “ Eeeee muone mama yakooo ana jicho moja” Maneno yale yalizidi kuongeza kichwani mwangu nilitamani ardhi ipasuke niingie na inifunike. Na wakati mwingine nilitamani mama atoweke kabisa nisimuone maishani mwangu. Mama aliposogea karibu yangu nilimtwanga swali “Hivi wewe mwanamke unanipenda kweli?” mama yangu akajibu “Ndioo mwanangu nakupenda sana tena zaidi ya sana kwani wewe ni mtoto wangu pekee na sina mtoto mwingine zaidi yako, wewe ni lulu moyoni mwangu na dhahabu machoni pangu na wewe ndio furaha ya maisha yangu” kwa hasira huku nikifoka nikamwambia kama kweli unanipenda kwa nini usife ili mimi nikawa na raha hapa duniani?. Mama yangu hakujibu kitu kwa wakati ule….

Akaamua kuondoka machoni pangu kimya kimya! Mimi wala sikuona kama lile lilikuwa kosa na wala sikufikilia na wala sikupata walau hata nukta moja ya kutafakari nini ninachokifanya, sababu nilikuwa nina hasira sana. Ukweli nilikuwa sitambui mawazo yake mama na nilikuwa sijui nini mama anavyowaza juu yangu. Na kwa vile sikuwa na lakumfanya kwa wakati ule baada ya yeye kutoka mle ndani nami nikatoka nje huku nikiwa na mawazo sana. Nilikuwa nasoma kwa bidii sana, na baada ya mtihani wa mwisho nikapata bahati ya kuchaguliwa kuendelea na masomo ya juu jijini Dar es salaam. Hivyo kwa nguvu ya shule nilisafirishwa kutoka Mbeya mpaka dar, mama alinipatia pesa za matumizi pindi nitakapokuwa dar! Kwa jinsi alivyokuwa ananipenda alinipa mshahara wake wa miezi mitano, kumbe alikuwa ananitunzia hata kabla matokeo hayajatoka. Nilifurahi sana ingawa sikumshukuru lakini mama hilo hakujali alifurahi sana vile ambavyo nilipokea zile pesa kisha akanitakia safari njema. Nilipofika dar nikaendelea na masomo yangu kama kawaida. Kwa bahati pia nikafauru vizuri kisha nikaajiliwa Serikalini, Maisha yangu yalikuwa mazuri sana. Nilijenga nyumba nzuri ya kifahari nikanunua gari ya kutembelea ilikuwa gari aina ya Land cruzer mayai.

Sio siri maisha yangu yalikuwa mazuri sana. Baadaye nikaamua kuoa mke, tukazaa watoto watatu, familia yangu ilikuwa na furaha sana, sikuacha kuwasiliana na walimu wangu wa mbeya katika ile shule ya watoto yatima niliyokuwa nikisoma hapo awali, na kwa vile kwa wakati huo nilikuwa na pesa za kutosha nilikuwa natuma misaada katika shule ile. Ila mama sikuwahi kutuma hata shilingi kumi. Kwani nilikuwa natamani afe ili asiendelee kunitia aibu. Mama baada ya kupata habari kuwa mwanae maisha yangu yamekuwa mazuri na pia alisikia kuwa nimeoa na pia nimezaa watoto alifurahi sana na alitamani sana kuwaona wajukuu zake. Kwa wakati huu mama yangu alikuwa ameanza kuzeeka na aliamua kuacha kazi yake ya upishi katika ile shule. Pamoja na kuwa alikuwa ni wanamke aliweza kujijengea kakibanda ka kujisitiri na kwa vile alikuwa ameitumikia shule kwa muda mrefu hawakuacha kumtunza, pia waliendelea kumpa mshahara wake kama kawaida maisha yakawa yanasonga. Kwa upande wangu sikutaka hata kusikia habari zake. Siku moja mama akaamua kunifuata Dar, ili walau awaone wajukuu zake na hata mie mwanaye kwani alikuwa hajaniona zaidi ya miaka ishirini na mbili hivi, akapanda basi na kuja dar kwa bahati alipofika dar alimpata msamalia mmoja aliyeweza kumsitiri kama mjuavyo jiji la dar jinsi lilivyo na zamani ilikuwa kutoka mbeya hadi dar unatumia siku mbili na kwa vile alikuwa amefika usiku hakujua ni wapi aelekee.

Siku iliyofuata aliamua kunitafuta kwa kuulizia na kwa vile mimi nilishakuwa mtu maarufu sana hakupata shida kuipata nyumba yangu. Alipofika Getini alibisha hodi, na mlinzi baada ya kumhoji na kupata maelezo alimruhusu aingie, alipokuwa akikaribia mlango wangu, niliwasikia watoto wangu wakipiga kelele huku wakimcheka mama yangu na kusema “Heee! Cheki hicho kibibi kizee chongo kimekuja kwenye birthday party ya baba bila kualikwa” kusikia hivyo nkatoka nje na nikamuona mama akija wakati huu alionyesha wazi kuwa alikuwa mdhaifu! Ingawa hatukuonana kwa muda mrefu sana, sikuwa na hata chembe ya kumkumbuka. Nilifoka na kumwambia “ We kizee wewe unathubutuje kuja humu ndani na kuwashitua watoto wangu? Hauna hata haya tafadhari sana naomba uondoke haraka hapa.” Tokaaa!! Mama aliniangalia kwa huruma sana huku machozi yakimlengalenga katika macho yake, kisha akasema “Samahani kijana wangu nimekosea nyumba aliyenielekeza alinielekeza vibaya! Naomba unisamehe sana! Akageuka na kuanza kuondoka, haimaanishi kuwa hakunitambua alifanya vile ili kuuridhisha moyo wangu!.. hivyo akatoweka machoni pangu wala kuumia moyo kwa mama sikupata shida. Mama alikwenda moja kwa moja stendi ya mabasi kukata ticketi ya kurudi mbeya. Wakati ule ilikuwa manazi mmoja.

Akalala kwenye basi kesho yake akaanza safari ya kurudi Mbeya. Siku moja nilipokea barua kutoka katika ile shule niliyokuwa nikisoma ya watoto yatima, wakinihitaji niende huko kulikuwa na sherehe iliyoandaliwa ya kuwakutanisha wanafunzi wote waliosoma miaka ya nyuma ambao wamekuwa bega kwa bega katika kuisaidia shule ile. Kwa hiyo hata mie nilikuwa mmoja wao, na kwa vile nilijua kuwa nakwenda ni nyumbani sikutaka mke wangu amfahamu mama yangu na pia sikutaka mke wangu ajue kuwa nilisoma shule ya watoto yatima hivyo nikamuaga kuwa naenda Mbeya kikazi kwani siku zote mke wangu nilimwambia kuwa mie ni mzaliwa wa Dar na sina ndugu kabisa wazazi wangu wote wawili walifariki zamani sana. Siku iliyofuata nikaanza safari yangu kuelekea nyumbani kwetu mbeya, wakati huu nilikuwa nawaza jinsi ambavyo ningepokelewa kwa furaha pale shuleni lakini nilikuwa napata shida sana kwamba naenda kukutana na mama yangu ambaye alikuwa kero sana kwangu. Sikumpenda sana mama yangu hasa kwa lile tatizo lake la kuwa na jicho moja. Nilifika salama mbeya na kwa vile nilikuwa nimetumia usafiri wangu nilifika mapema kabisa, nikaenda katika moja ya nyumba za kulala wageni iliyokuwa bora sana nyumba yenyewe ilikuwa ikiitwa Mount Livingstone Hotel. Basi kama ilivyo ada nikaamka asubuhi na kujiandaa tayari kwenda kwenye sherehe.

Nilipofika kwenye sherehe kulikuwa na maclassmet kibao walikuwa wamefika pale na pia walikuwa na wake zao na hata wale waliokuwa ni madada zetu walikuwa wamekuja na waume zao, pamoja na hayo yote walikuwa wamekuja na wazazi wao karibu kila mmoja alikuwa na mzazi japo mmoja. Kwa upande wangu nilikuwa peke yangu, zaidi sana nilikuwa nimeambatana na dereva wangu tu. Lakini halikunipa shida hilo na nilikuwa nimeshukuru sana mama yangu kutokuwepo pale kwenye sherehe. Sio siri sherehe ilikuwa imefana sana na ilikuwa ni ya aina yake. Baada ya sherehe tukaendelea kusalimiana na wale wazee wa pale kijijini wote tukiwa na furaha sana. Baadaye akaja yule mama aliyekuwa rafiki yake na mama yangu akaniambia “pole sana mwanangu kwa msiba wa mama yako” Msiba wa mama? Nilimtwanga swali kuonekana kana kwamba nimeshituka, ingawa nilijua wazi yule mama alikuwa anajua tabia yangu na yale yote niliyokuwa nikimtendea mama yangu! Yule mama akasema “ndioo mama yako alikufa mwezi week mbili zilizopita ina maana hukupata taarifa? Nikamjibu sikupata taarifa. Basi tuakaendelea na mazungumzo mengine, ila kusema ukweli ile taarifa ilinifurahisha moyoni mwangu nikajua kuwa kero yangu sasa imekwisha. Hata hivyo mwisho wa mazungumzo yule rafiki wa mama yangu aliniita pembeni na kuniomba niambatane naye kwenda nyumbani kwake, nami bila hiyana nikakubali kwenda.

Tulipofika nyumbani kwake aliingia chumbani kwake na kutoka na barua akanipatia ile barua na kuniambia kuwa mama yangu alisema anipatie mimi….. Nilipokea ile barua kuanza kuisoma ilikuwa imeandikwa hivi:- Kwa Mwanangu Kipenzi, Nimekuwa nikikuwazia wewe wakati wote, sababu nakupenda sana, Naomba unisamehe sana kwa kuwatisha watoto wako siku ile niliyokuwa nimekuja kwako Dar, naomba nisamehe sana mwanangu, nisamehe sana. Nimepata furaha sana kusikia kuwa utakuja huku kwenye sherehe ya shule yenu, lakini najua kuwa sitakuwepo kwenye sherehe hiyo, kwani sipendi kukukwaza mwanangu. Ila mwanangu najua nimekukwaza kwa muda mrefu lakini haikuwa malengo yangu ilikuwa ni kwa sababu ya upendo niliokuwa nao kwako na vile nilivyopata tabu sana kukupata kwani wewe ndiwe mtoto wangu wa pekee. Sikia mwanangu…… nataka ufahamu haya… Wakati ukiwa angali bado mdogo ulipata ajali na kupoteza jicho lako moja na mimi kama mama yako sikupenda kukuona mwanangu ukikua huku ukiwa na jicho moja hivyo nikaamua kutoa jicho langu moja na kukuwekea wewe, ili ukue huku ukifurahia ulimwengu huu mpya ukitumia kiungo changu ambalo ndiyo jicho nililo kupatia. Nilikupenda sana mwanangu nab ado nakupenda sana! Ni mimi mama yako!! Mwisho!.. NB: Ni stori tu ila kuna watu wana tabia za kuwadharau wazazi hususani mama zao naomba kwa hali yoyote ile mpende mama yako, hakuna aliye kama mama hapa Duniani!!! Nampenda sana mama yangu

FRIENDS CHANGE TIME AFTER TIME

Usiwe na Mashaka na Hofu unapopoteza rafikia au Marafiki ..Mungu huwa anakupa marafiki fulani kwa kipindi fulani maalum ili wakusaidie wewe kupita kwenye kipindi hicho..Ukivuka hiyo stage anakupa marafiki wengine ambao ni specific kwa stage mpya uliopo..Usiforce rafiki wa Stage 1 abakie kwenye Stage 2 kama he is not meant to stay..Let him go,ha-fit kwenye purpose!..Ndio maana kuna mtu alikuwa besti sana shule lakini sasa hv hayupo tena,kuna mtu kaletwa kwa stage hii...

Divai mpya haiwezi kuwekwa kwenye kiriba kikuu-kuu,lazima kitapasuka...Ukiforce Old friend awepo kwenye new life kuna mambo mawili,aidha You loose ur Purpose ya Mungu kukuweka kwenye hiyo Stage au you loose that friend ili Purpose yako iwe accomplished...Say goodbye to all friends who block ur Purpose to be accomplished and let God give you the right people to help you reach your destiny...

KWA WANAWAKE WENYE AKILI, KAMA HUNA AKILI USISOME

Kama kuna mwanaume amekuacha bila sababu yoyote ya msingi,au ametafuta kasababu ka kijingajinga tu ili abreak up,amepata mwanamke mwingine.Ukaumia,ukalia,ukapona,ukapata mtu mkaanzisha mbingu yenu yenye amani na raha,GHAFLA yule furushi aliyekuacha anaanza kurudi,mara akosee message, atume kwako,mara anajikomba kuomba msamaha kurudi baada ya kuona kule mambo sio,eti shetani alimpitia,kwani siku hizi Shetani ana gari hadi ampitie yeye tu?KAMWE usilambe matapishi.
Usikubali kugeuzwa ARV,vile vidonge,ili umuongezee maisha yeye baada ya kukumbana na virusi vya kuachika huko alikokimbilia kwa mbwembwe.Mwanaume ni msimamo,kama alikuacha kwa sababu,ukikubali kumrudia tena ipo siku atapata sababu tena ya kukuacha na utaumia mara mbili...

UKITAKA KUMJUA MSICHANA AMBAEHAKUTAKI,HAYA NDIO MAJIBU YAKE

1.Baby 2taongea badae,nna kazi nyng
2.Jamani honey ckuweza kupokea cm nilikua kwenye kelele.
3.Sweety cna credit,that's why cjajibu sms yako.
4.2ko discussion,ntakubep badae dear.
5.Cm haikua & chaji jamani (hapo alikuzimia cm).
6.Nipo na kaka yangu,ucpige sim.
7.Naumwa,kesho ha2wezi kuonana.
8.Room mtu wangu anamgeni,ucje leo.
9.Nipo safarin,ntakutafuta badae (kwa saut ya chini).

"SOMA HII KI2 UFURAHI KIDOGO"

Jamaa alipeleka gari lake kwa fundi lipakwe rangi!
Fundi akauliza lipakwe rangi gani?
Jamaa akasema yeyote isipokuwa nyekundu, nyeupe, bluu, njano, kijani wardi, nyeus, chocketi, kijivujivu, maziwa, zambarau, orange na nyingi nyengnezo akazitaja!
Lini nije kulichukua gari langu?
Fundi akamjibu "Njoo cku yoyote icpokuwa Jumatatu, Jumanne, Jumatano, Alhamis Ijumaa, J'mosi wala jumapili!

YUPI MKALI

Wachungaji 3 walikutana waelezane matatizo yao ili waweze kuombeana wa kwanza akasema jamani mimi tatizo langu wizi yaani kila nikimaliza ibada lazima niibe hela za sadaka,Wapili akasema jaman mimi tatizo langu napenda wanawake yaani kila mwanamke nataka kulala nae nimeshatembea na wanakwaya wote,Watatu badala ya kuongea akaanza kulia wenzie wakamuuliza unalia nini? Akajibu, "jamani mimi tatizo langu umbea yaani haya yote tuliyoongea lazima nikaseme"!

AIIIIIIIIIIII MWANAMKE LAZMA ADANGANYWE

...daaa kuna demu mmoja nilimdanganyaga naxoma chuo IFM kumbe na yy anasoma pale pale
Kesho yake asubuhi na mapema akaja kunipitia twende chuo akamkuta mama

Demu......shikamoo mama
Mama cox......marahaba binti hujambo
Demu......sijambo mama nimemkuta cox dawa yao
Mama cox.....ndo nan huyo mbna mm simjui alikuambia anakaa hapa?
Demu......ndiyo ni mkaka mmoja hivi mfupi ana kichwa kikubwa anapenda sana kuvaa tishet ya voda
Mama cox.....ahaaa huyo ni mwanangu anaitwa CHOGO NDIZI sio COX DAWA YAO hilo jina kakudanganya una shida naye??
Demu....duuu ndiyo nimempitia twende chuo
Mama cox.....uwww chuo gani tena kashakudanganya yupo chuo muongo yule mwanangu kashazoea kudanganya wanawake anawapa sana mimba watoto wa watu hana lolote hasomi wala nn tumempeleka chuo cha ufundi cherehani kakataa sasa hivi anatengeneza baiskeli mbele hapo
Demu ....daaa kweli mama
Mama cox....twende nkupeleke anapotengenezea baiskeli

Daaa mama kamleta hadi kilingeni demu kanikuta naziba pancha nimetupa tairi nimetoka nduki sina hamu aisee nimelia sana mama kaniharibia demu kanitukana sana kwenye simu daaa

WATANZANIA KWA KUPENDA SIFA.

Mtanzania, Mnyarwanda, na Mkenya walikamatwa na madawa ya kulevya China. Wakaambiwa adhabu ni mbili kifo au adhabu nyingine ambayo wakiishindwa pia wanauawa. Wakaomba wapewe hiyo adhabu nyingine wajaribu bahati yao. Wakapelekwa msituni wakaambiwa waingie msituni kila mmoja kwa njia yake halafu kila mmoja arudi na matunda kumi ya kufanana. Wakaingia msituni kila mtu njia yake. Mnyarwanda akarudi wa kwanza. Karudi na maepo kumi. Akaambiwa adhabu ni kuyameza yote mazima mazima moja baada ya jingine bila kufumba macho bila kulia wala kucheka wala kujitikisa! Akameza la kwanza. Safi. Kumeza la pili akashindwa kuvumilia akafumba macho. Akapigiwa risasi akafa.
Wa pili Mkenya akaja. Ana vitunda vidogo vidogoo. Kumi. Vya kufanana. Vidogo kama pipi. Akaambiwa masharti. Akaanza kula bila kufumbua macho wala kulia wala nini. Alipofika cha tisa akashindwa kuvumilia akaangua kicheko! Akapigwa risasi pia akafa. Wakiwa kuzimu Mnyarwanda akamuuliza Mkenya.. "Vipi wewe mbona ulishindwa kuvumilia wakati ulibakisha kitunda kimoja tu?" Mkenya akajibu: "Kaka, nilishindwa kuzuia kicheko maana nilimwona Mtanzania anakuja na matikiti maji!".....

Thursday, April 4, 2013

FAIDA YA KUMFAGILIA MUPENZI WAKO KWA MAMBO YA NDANI NA YA NJE ANAYOKUFANYIA!


mengi mazuri ambayo huenda mpenzi wako aliwahi kukufanyia, je uliwahi kumshukuru kwa kukufanya ufarijike? Naamini Mungu amekujaalia kuwa na mpenzi mzuri, mwenye kila sifa ambayo
ulitamani awe nayo, je ulishawahi kumsifia hata kwa kumwambia ni mzuri?
Huenda ulishawahi kufanya hivyo lakini kwa taarifa yako wapo ambao wanahisi kufanya hivyo eti ni ulimbukeni. Ulimbukeni? Kumsifia mpenzi wako unaona ni ulimbukeni wakati wataalam wa masuala ya mapenzi wanaeleza kuwa, wanawake ni watu wanaopenda kusifiwa sana hata kwa madogo wanayoyafanya?
Unaona hatari gani kumsifia mpenzi wako kuwa ni mzuri? Unadhani unatumia nguvu gani kumsifia mpenzi wako kutokana na mahaba mazito anayokupata? Kwa taarifa yako unaweza kuona ni kitu kidogo sana lakini
madhara yake kwenye penzi ni makubwa.Kumsifia mpenzi wako kwa yale anayokufanyia kuna faida nyingi sana lakini kwa leo nitagusia chache Kwanza kunaongeza mapenzi. 

Mume/mke anaposifiwa kuwa anajua mapenzi hata kama si kwa kiwango kikubwa, anafarijika sana. Unapomwambia mpenzi wako: ‘Dear nashukuru kwa mapenzi uliyonipa jana, umenipa furaha ya ajabu ambayo siamini kama kuna mtu mwingine wa kunipa, nakupenda sana’. Maneno kama haya hutumii
nguvu wala muda mwingi kuyafikisha kwa mpenzi wako lakini uzito wake ni mkubwa. Kwanza anajihisi aliyekamilika kwa kufikia hatua ya kufanya mambo yakamridhisha mpenzi wake na kwa mazingira hayo anaamini huwezi kumsaliti. Hisia hizo zitamfanya azidi kukupenda. Hilo ni kwa wote yaani kwa mwanaume na mwanamke. Lakini pia unapomsifia mpenzi wako kwa yale anayokufanyia, unamfanya aongeze kasi ya
kukufanyia ili nawe uzidi kumpenda. Kwa mfano, unapokutana na mpenzi wako kisha ukamwambia ‘umependeza kweli mpenzi wangu, nazidi kukupenda kwa unavyovaa’. Mtu anayeambiwa maneno haya
atajitahidi sana siku zote aonekane nadhifu na wa kuvutia kwa mpenzi wake akijua kwamba, akivaa ilimradi kuvaa hatamfurahisha mpenzi wake. Kwa maana hiyo kumsifia mpenzi wako kunamfanya azidi kuwa bora. Lakini kusifia kusiwe kwa kinafiki. Usimsifie mpenzi wako eti ili kumfanya ajione bora kumbe katika uhalisia siyo hivyo.

 Tusifiane pale inapobidi huku tukijua kuwa kwa kufanya hivyo tutapata faida. Tusiwe na tabia ya kuchukulia poa kila tunachofanyiwa na wapenzi wetu. Kama kakuridhisha kimapenzi, msifie kwamba yeye ni muhimu kwako kwa kuwa amekupa ulichotarajia. Amekupikia chakula kizuri, msifie kuwa yeye ni mpishi mzuri. Hiyo italinogesha penzi na utashangaa kila siku inayokwenda kwa Mungu penzi lenu linachanua.
Lakini mbali na hayo, unatakiwa kuridhika kwa kile unachokipata kutoka kwa huyo mpenzi wako ulinaye kwa sasa. Najua kwenye uhusiano wengi tumetoka mbali. Wapo waliowahi kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja huko nyuma na kila mmoja alikuwa na kiwango chake cha kukuridhisha. 

Inawezekana kuna ambaye unamkumbuka kwa mapenzi mazito aliyokuwa anakupa zaidi ya huyo uliyenaye. Hiyo ni historia, imepita! Kama huyo uliyenaye si mtaalam sana wa kukufikisha pale unapopata, ridhika na hicho kidogo unachokipata endapo atakuwa anaonesha kukupenda kwa dhati.Mpe moyo, msifiesifie kidogo kwa hiyo furaha kiduchu anayokupa huku ukiamini kuwa, atabadilika kadiri siku zinavyokwenda.
Kumbuka cha msingi katika maisha yetu ni kumpata mtu mwenye mapenzi ya kweli na si kumpata anayeweza kukuridhisha katika mambo kadha wa kadha.

WHY DO MEN LIE???


Hahahahaaaa!!!! Mniruhusu nicheke kwanza....
Girls, you wanna know????
Sababu chache kwanini Wanaume ni waongo hizi hapa:

1. WANAJUA
Uongo wa Mwanaume ni kama muvi...Kabla hajadanganya anapanga angle zote na majibu,ana-anticipate ataongea nn,utamjibuje,utamuuliza nn,na atakujibu nini...Wanawake hamuwezi,huwa mnapanic,na siku zote ukipanic umefeli

2. HATA TUKISEMA KWELI
MNADHANI TUNADANGANYA
Hii ndo ilivyo,na inaudhi...Kwa sababu tunadanganya sana,hata pale tunaposema kweli basi nyie mnatuona wezi...So hakuna maana kusema kweli,bora tuendelee na PHD ya uongo tu-graduate

3. WANAWAKE WANAPENDA UONGO
Japo hawasemi lakini hili tumeliprove,Wanawake ukimwambia uongo ndo anapenda...whether kwa kujua au kwa kutokujua...Ukimwambia ukweli anakuona hamnazo...Ukimwambia Mwanamke kweli Utajuta....Itakuwa ndo wimbo bora wa mwaka...Masimago na Rewind button...Mwaka mzima,ukikosea tu wanarewind ulichokiri..Waulize Wanaume waliowahi kukiri kucheat wakusimulie,wanajuta kwanini walikuwa na mahaba kuliko

4. UONGO KWENYE MAPENZI NI NDIMU KWENYE SUPU
Mapenzi ni sanaa na sayansi....Mapenzi sio engineering! Kama ndimu kwa supu ndivyo Uongo kwenye mahaba...kuna vitu unajua umedanganywa lakini unatolewa macho makavu inabidi uwe mpole..inabaki kama drama,na inaleta ladha flani ambayo ni ngumu kuielezea,japo wanawake wanaweza kuielezea how they feel pale ambapo wanajua wamedanganywa lakini hawana proof kwamba ule ni uongo...Mwanaume anashinda kirahisi...inabakia kama assignment flani hivi kwa Mwanamke kwamba next time lazima awe wise kidogo
kumkamata...Na hiyo ndo ladha yenyewe na vionjo vya mahaba
SISEMI MDANGANYE,ILA NDIMU KIDOGO TU SUPU IPATE KUKUPA HAMU

TAMBUA JINSI YA KUONGEA NA MPENZI WAKO ANAPOKUWA AMEKASIRIKA.


Kwenye mapenzi kuna nyakati za kutofautiana na kukasirishana. Katika hali ya kawaida, kipindi hiki huwa ni cha hatari kwa sababu husababisha ufa mkubwa wa uhusiano na kulifanya penzi kukosa ladha.
Sote tunajua kuwa watu hupigana, huachana, hujeruhiana, hutukanana na hudhalilishana wakiwa na hasira. Hata hivyo, si wote wanaojua wafanye nini wanapoingia kwenye hatua hiyo mbaya.Ndugu msomaji wangu,
hebu jaribu kukumbuka ugomvi mmoja uliotokea kati yako na mpenzi wako na ikiwezekana jikumbushe mlivyoanza! Utabaini kuwa mlianza kama utani na mkajikuta mmefura kwa hasira, mkatwangana makonde, mkatamkiana maneno makali ya kuudhi na pengine mkaamua kuachana. Yote hii ni kwa sababu mlikosa elimu ya mazungumzo. Ingekuwa mmoja wenu hasa yule aliyekuwa wa pili kukasirika anafahamu hatua za kuzungumza na mtu aliyekasirika angechukua jukumu la kutuliza machafuko na kuleta amani kwenye mapenzi.

Zifuatazo ni hatua tano za kuzungumza na mpenzi aliyekasirika:

1. MPUNGUZE MHEMKO
Hasira hujaza kifua, huathiri mzunguko wa damu na ufahamu. Mtu aliyekasirika huwa vigumu kwake kusikiliza au kutazama mambo kwa jicho la tatu. Mwenye hasira huwa hafikirii matokeo yajayo badala yake hutazama zaidi tukio na jinsi ya kupata ushindi, iwe kwa maneno au kwa mapambano. Katika hali ya namna hiyo, mtu mwingine akija na busara za kutaka kumgeuza haraka haraka hawezi kumuelewa. Jambo la muhimu hapo ni kuacha kumwandama, kujibizana naye au kumshawishi akusikilize. Badala yake mpe nafasi ya kusema atakavyo, abwate ajuavyo huku wewe ukimuitikia na kumkubalia lawama zake.“Basi mpenzi mwenye makosa ni mimi.” Kauli za aina hii zitampunguza hasira kwani atajiona mshindi.

2. MSOME SAIKOLOJIA YAKE
Kwa kuwa unamfahamu mpenzi wako kwa kina, itakuwa rahisi kwako kumtambua kuwa amepunguza hasira na kurudi katika hali yake ya kawaida. Ukilifahamu hilo chukua jukumu la kumsoma kisaikolojia ili kujua kama yuko kwenye hali nzuri ya kusikiliza yale uliyotaka kumwambia wakati alipokuwa na hasira.
Zoezi hili linaweza kuchukua saa kadhaa na wakati mwingine hata siku mbili. Lengo ni nini? Ni kupata matokeo sahihi ya kuondoa chuki za mwenza wako na kumfundisha madhara ya kukasirika kwenye uhusiano wenu wa kimapenzi. “Nakupenda sana, lakini juzi uliniumiza, uliniambia mimi malaya kwa kosa ambalo sikulifanya” Bila shaka muda huo atakusikiliza zaidi kuliko ungebishana naye alipokuwa na hasira.

3. MRUHUSU AKUJIBU
Pamoja na kumsoma kisaikolojia na kumwambia kinagaubaga makosa yake, usimzuie kujitetea. Mpe nafasi ya kuzungumzia kilichomkasirisha. “Unaona bado unanitukana, sasa naamini siku ile ulikuwa umedhamiria.” Usisiseme hivyo, mwache ajibu hoja hata kama atakuwa anakukandamiza na kuzidi kujijengea ushindi Mvumilie aoshe ubongo wake.

4. EPUKA MALUMBANO
Kama nilivyosema hapo juu, wapenzi wengine huwa wagumu kuelewa, ni watu wa kuficha udhaifu wao na kutopenda kuonekana wamekosea. Watu wa namna hii unapowarejeshea mazungumzo wanaweza kuhamaki tena. “Kwa hiyo ulikuwa unasemaje… nilifanya ndiyo,… wewe unaamuaje?” Mkifika kwenye hatua kama hiyo usikubali kulumbana naye, muache aseme halafu wewe ingia kwenye hatua ya tano.

5. MUOMBE MSAMAHA
Hata kama atakuwa yeye ndiye mwenye makosa na amekataa kukiri, usijali, chukua jukumu la kumuomba msamaha na kueleza tena nia yako ya kuzungumza ilikuwa ni kuelewana si kugombana. Kumbuka hata kama amekiri kosa, bado unatakiwa kumuomba radhi kwa kurejea yaliyopita.
“Mpenzi inawezekana nikawa nimekuudhi kwa niliyoyasema, nakuomba sana tusameheane.”

Bila shaka kwa haya machache utakuwa umejifunza na kuchukua hatua za kuzuia migogoro
mikubwa inayotokana na hasira za mpenzi wako.