Friday, May 3, 2013

HAHAHAHA KAMA NI WEWE UNGEFANYA NINI?

Jamaa mmoja alipata mchumba akaona ni vyema amtambulishe kwa baba yake, mzee alipomuona tu akasema, "oho huyu ni dada yako ni mtoto wangu huyu nilizaa kipindi niko shule", jamaa akatafuta mchumba mwingine akafanya vile vile lakini mzee akasema "oho ulimufahamu vipi huyu ni dada yako pia" jamaa akaona isiwe shida akatafuta kimwana mwingine, digi alipopelekewa na huyo akasema "aha sasa ww mtoto kwanini unakuwa unakutana na dada zako tu, huyu naye ni dada yako tafuta mwingine ila usimwambie mama yako maana hajui kama nina watoto hawa", 
jamaa akawa na hasira sana akaenda kumpatia story yote mama yake, mama akamwambia "aha hata usijali hao sio dada zako hata kwa damu maana hata wewe huyu sio baba yako ila usimwambie maana hajui ni siri yangu ya muda mrefu, wewe fanya kuchangua unayempenda kati ya hao uoe.

No comments:

Post a Comment